Watumiaji Wa Iphone Wataweza Kutuma Sms Sehemu Isiyo Na Mtandao

Watumiaji Wa Iphone Wataweza Kutuma Sms Sehemu Isiyo Na Mtandao

Apple, SpaceX, na T-Mobile wameungana katika ushirikiano wa kimkakati ili kuboresha mawasiliano kwa watumiaji wa iPhone.

Kupitia ushirikiano huu, iPhone zenye toleo jipya la programu (iOS 18.3) sasa zinaweza kuunganishwa na mtandao wa ‘setilaiti’ wa Starlink wa SpaceX, kupitia huduma ya T-Mobile.

Ambapo watumiaji hao wataweza kutuma ujumbe wa maandishi kupitia setilaiti za Starlink hata wakiwa katika maeneo ambayo hayana mtandao wa kawaida wa simu.

Aidha baada ya kufanikiwa hilo waunganishaji wa Setilaiti hiyo wanaeleza kuwa kwa sasa wanawekeza zaidi nguvu zao ili watumiaji wa program hiyo waweze kupiga simu na kutumia data hata sehemu zisizo na mtandao siku zijazo.

Kwa sasa huduma hii inapatikana wa watumiaji wa Apple wa Marekani huku kukiwa na matarajio ya kupanua huduma hiyo iweze kusambaa kimataifa.






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Aisha Lungato

A digital journalist and writer for Mwananchi Scoop. My stories are around entertainment, lifestyle, artist profiles and career.


Latest Post

Latest Tags