Tyga Athibitisha Kufiwa Na Mama Yake

Tyga Athibitisha Kufiwa Na Mama Yake

Rapa kutoka Marekani Tyga amethibitisha kutokea kwa kifo cha mama yake mzazi aitwaye Pasionaye Nicole Nguyen, ambaye amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 53

Tyga amethibitisha taarifa hiyo kupitia ukurasa wake wa Instagram huku akiweka wazi huzuni anayopitia kwa kumpoteza mtu muhimu katika maisha yake.

“Nimekuwa nikijaribu kuelewa na kushughulikia kwa nini Mungu huwachukua watu wenye maana zaidi na waliopendeza zaidi kutoka kwetu. Lakini najua sitawahi kupata jibu litakalojaza pengo lililo moyoni mwangu. Siwezi kufikiria maisha bila wewe kando yangu. Ulikuwa mtu bora na mwenye msaada mkubwa zaidi maishani mwangu, ulinifanya nijihisi vizuri hata nilipokuwa katika hali yangu mbaya zaidi. Ningetoa chochote ili tu niwe nawe tena.

Nakupenda Sana, na siwezi kusubiri siku tutakapokuwa pamoja tena, Nitakuona hivi karibuni, tafadhali niwekee nafasi karibu nawe peponi. Nakupenda milele mama, na nitajitahidi kukusherehekea katika kila muda nitakaobakiwa nao. Pasionaye Nicole Nguyen 9/11/71 - 1/18/25,” ameandika Tyga






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Aisha Lungato

A digital journalist and writer for Mwananchi Scoop. My stories are around entertainment, lifestyle, artist profiles and career.


Latest Post

Latest Tags