Waigizaji na wachekeshaji maarufu kutoka Marekani, Eddie Murphy na Martin Lawrence wameripotiwa kuwa ndugu baada ya mtoto wa Eddie, Eric Murphy, kufunga ndoa na binti wa Martin, Jasmin Lawrence.
Wakati alipokuwa kwenye mahojiano na ‘The Jennifer Hudson Show’ Murphy alithibitisha kuwa watoto hao walifunga ndoa ya siri kanisani wiki mbili zilizopita.
“Martin sasa hana tena mzigo wa kugharamia harusi kubwa. Watoto wetu walifunga ndoa kwenye ibada ya faragha, wao wawili tu na mchungaji. Hakukuwa na harusi kubwa,” Amesema Eddie Murphy
Hata hivyo mwigizaji huyo aliendelea akiweka wazi kuwa wanandoa hao wapya wanampango wa kufanya sherehe kubwa siku zijazo. Wawili hao walianza uhusiano wao mwaka 2021 na kutangaza uchumba wao mwishoni wa mwezi Novemba 2024.
Utakumbuka Eddie Murphy na Martin Lawrence wameonekana katika filamu mbalimbali ikiwemo Life (1999), Coming to America (1988), Big Momma's House (2000), Blue Streak (1999), Beverly Hills Cop (1984) na nyinginezo.

Leave a Reply