Mwalimu Wa Hesabu Aogelea Kwa Miaka 20 Aweze Kufika Shule

Mwalimu Wa Hesabu Aogelea Kwa Miaka 20 Aweze Kufika Shule

Mwalimu Abdul Malik maarufu kama ‘Tube Master’ mwenye umri wa miaka 42 kutoka nchini India amekuwa akiwavutia wengi kufuatia na kujitoa kwake, ambapo kwa takribani miaka 20 amekuwa akipita njia yenye mto kwa kuogelea ili aweze kufika kazini katika Shule ya Msingi ya Kiislamu ya Padinjattumuri.

Kwa mujibu wa tovuti mbalimbali, Mwalimu huyo huchagua kuogelea kwa kuvuka mto ili kuepuka safari ya kilomita 24 kwa barabara, ambayo inamhitaji kubadilisha mabasi matatu na kuchukua muda mrefu kufika shuleni.

Mwalimu Malik huanza siku yake kwa kuogelea akiwa na mfuko wa plastiki anaobeba nguo zake na vitabu, na baada ya kuvuka mto, hubadilisha nguo na kuendelea na safari ya kuelekea shuleni. Licha ya changamoto hiyo ya kila siku, hajawahi kukosa darasa hata siku moja, akionesha kujitolea kwa hali ya juu katika taaluma yake.



Aidha mpaka mwishoni mwaka mwaka 2023 mwalimu huyo aliendelea kuvuka mto lakini baada ya kupandishwa cheo na kupewa majukumu mapya sasa hutumia barabara kufika shuleni.






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Aisha Lungato

A digital journalist and writer for Mwananchi Scoop. My stories are around entertainment, lifestyle, artist profiles and career.


Latest Post

Latest Tags